NANI kati wa washiriki 17 ataibuka
kuwa mshindi wa shindano la Redd's
Miss Temeke 2014, linalofanyika kesho
kwenye Ukumbi wa TCC Club
Chang'ombe Dar es Salaam.
Jumla ya warembo 17 kutoka vitongoji
vya Mbagala, Kurasini na Chang;ombe
watapanda jukwaani kuwania taji hilo,
huku washindi wa tatu watapata
nafasi ya kushiriki shindano la Miss
Tanzania mwaka 2014.
Akizungumza Dar es Salaa jana
Mkurugenzi BMP Promotions, Benny
Kisaka, alisema kuwa maandalizi ya
shindano hilo yamekamilika kama
yalivyopangwa.
Kisaka alisema kuwa taji
linaloshikiliwa na mrembo kutoka
kanda ya kati, lakini mwaka huu
Temeke imejizatiti kutoa si tu Miss
Tanzania, mbali warembo watatu wa
kwanza wa Taifa kutokana na viwango
vya warembo wa mwaka huu.
Alisema kuwa mbali ya shindano hilo
kubwa, kulifanyika shindano dogo la
awali lililoandaliwa na Michuzi Media la
Miss Photogenic ambalo mshindi wake
atazawadiwa kitita cha Sh. milioni 1
taslimu, shindano ambalo lililsimamiwa
na jopo la wapiga picha wa kampuni
hiyo ambao watamtangaza na kumpa
zawadi mshindi siku ya shindano.
Kisaka aliwataja Warembo
wanaotarajiwa Subira Ally, Hellen
Yughin, Catherine Alex, Dalina David,
Winfrida Guntram, Salama Salehe,
Grace John, Lilian Lothy, Amina Salim,
Rebecca Mdamu, Sitti Mtemvu, Hellen
Sule, Neema Mollel, Lucy Lewis,
Esther Mnahi, Pauline Nkini na Patricia
Ponsian ambao walikuwa chini ya
ukufunzi wa Super Bokilo, Shadya
Mohamed na Sweet Remmy.
Alisema mkali wa bongofleva, Khalid
Mohamed TID almaarufu kama Top in
Dar, sanjari na Wanne Star, Makirikiri
wa Tanzania, Young Suma, Super
Bokilo na wasanii mbalimbali
wanatarajia kupamba shoo hiyo
ambayo Dj John Peter Pantelakis
atalisindikiza.
Wadhamini wa shindano hilo ni TBL
Kupitia Redds wamedhamini shindano
hilo sanjari na kinywaji cha Zanzi,
Michuzi Media Group, Radio EFM 93.7
Cash & Carry Distributors, Kitwe
General Traders, Rio Gym & Spa, CXC
Africa, 88. 5 Clouds FM, City Sports
Lounge, Gazeti la Jambo Leo, Kiwango
Security na 100.5 Times FM.
BMP Promotions imeshakamilisha
shindano hili la 19 tangu kuanzishwa
Miss Temeke chini ya undaaji wake
kwa asilimia kubwa, hivyo washabiki
wa Kanda ya Temeke na vitongoji
vyake watarajie mabadiliko makubwa
katika aina ya shindano la urembo
litakavyokuwa Ijumaa.
1996- Asela Magaka
1997- Miriam Odemba
1998- Khamisa Ahmed (Miss Temeke
anayeendea kujiita hivyo huko
Marekani)
1999- Ediltruda Kalikawe
2000- Irene Kiwia
2001- Happyness Sosthnes Magesse
super model Millen( Miss Tanzania)
2002- Regina Mosha
2003- Hawa Ismail ( Sylvia Bahame
first runner up and Miss Tanzania
same year)
2004- Cecylia Assey ( mrs Agrey
Marealle), first runner up Miss
Tanzania
2005- Seba Aggrey
2006- Jokate Mwegelo (Miss Tanzania
fisrt runner up), Irene Uwoya 1st
runner Temeke & 3rd runner up Miss
Tanzania
2007- Queen David ( Miss Tanzania
second runner up)
2008- Angela Lubala (top five Miss
Tanzania)
2009- Sia Ndaskoy (top five Miss
Tanzania)
2010- Genevieve Mpangala ( Miss
Tanzania)
2011- Husna Twalib
2012- Edda Sylvester
2013- Svetlana Nyameyo ( Latifa
Mohamedsecond runner Temeke and
first runner up Miss Tanzania)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...