Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando (wa pili
kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana,
kuhusu onyesho la muziki lililoandaliwa na kitengo cha huduma kwa
wateja kupitia Mradi wa 'Tunakujali' kwa ajili ya kukusanya pesa za
kuchangia shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Pongwe mkoani
Tanga, litakalowashirikisha wanamuziki nyota, Mzee King Kikii (wa pili
kushoto) na Banana Zorro (kushoto), litakalofanyika kesho Septemba 03,
katika viwanja vya Airtel Makao Makuu. Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma
kwa Wateja wa Airtel, Adriana Liamba.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana Liamba (wa pili
kulia), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana,
kuhusu onyesho la muziki lililoandaliwa na kitengo cha huduma kwa
wateja kupitia Mradi wa 'Tunakujali' kwa ajili ya kukusanya pesa za
kuchangia shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Pongwe mkoani
Tanga, litakalowashirikisha wanamuziki nyota, Mzee King Kikii (wa pili
kushoto) na Banana Zorro (kushoto), litakalofanyika kesho Septemba 03,
katika viwanja vya Airtel Makao Makuu. Kulia ni Meneja Uhusiano wa
Airtel Tanzania, Jackson Mmbando.
Mwanamuziki nguli nchini, King Kikii akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam jana, kuhusu ushiriki wake katika
onyesho la muziki lililoandaliwa na kitengo cha huduma kwa wateja
kupitia Mradi wa 'Tunakujali' kwa ajili ya kukusanya pesa za kuchangia
shule ya watoto wenye mahitaji maalum ya Pongwe mkoani Tanga,
litakalofanyika kesho Septemba 03, katika viwanja vya Airtel Makao
Makuu. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando
(wa pili kulia), ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel, Adriana
Liamba na Mwanamuziki nyota, Banana Zorro.
Kampuni Airtel Tanzania leo imetangaza kuanzisha mpango wa
huduma kwa jamii utakaowashirikisha wafanyakazi wake kujitolea na
kushiriki katika kuchangia na kusaidia jamiii nchini.
Mpango unategemea kuanza wiki hii unashirikisha wafanyakazi kutoka
katika vitengo mbalimbali utawawezesha wafanyakazi hawa kuandaa
shughuli zitakazowawezesha kukusanya fedha kwaajili ya kusaidia shule
mbalimbali ambazo zina mahitaji muhimu katika maeneo mbalimbali
nchini.
Mradi huu umezindulia rasmi na Kitengo cha huduma kwa wateja ndio
kitakuwa cha kwanza kushiriki ambapo wameandaa burdani ya musiki
itakayowashirikisha magwiji mahiri wa muziki nchini King KKii and
Banana Zoro inayotegeme kufanyika siku ya jumatano tarehe 3 septemba
2014 katika viwanja vya ofisi ya Airtel. Wafanyakazi wa Airtel na
watu mbalimbali kutoka nje wamealikwa kushiriki na kiasi cha pesa
kitakachopatikana kitaenda kuchangia shule ya watoto wenye mahitaji
maalum Tanga.
Akiongea kuhusu mpango huu Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson
Mmbando alisema” katika kushiriki kutatua changamoto mbalimbali
zinazozikumba jamii wafanyakazi wa Airtel wameona ni muhimu kuanzisha
mpango huu maalumu wa kusaidia jamii. Airtel kupitia mpango wake wa
huduma kwa jamii umeonelea ni vyema kutenga siku 14 mahususi kwa
wafanyakazi kupata muda wa kusaidia jamii.
Hivyo tutakuwa na shughuli
mbalimbali kuanzia sasa zitakazofanya na wafanyakazi katika kukusanya
fedha na kisha kufatiwa na siku 14 za kutoa misaada wa jamii
zinazotegemea kuanza rasmi mwakani mwezi wa tatu. Lengo letu ni
kuhakikisha tunazifikia shule 10 na kuzisaidia kwa sasa na leo
tunachukua nafasi hii kuwaalika wafanyakazi wetu na jamiii kutuunga
mkono na kushirikiana nasi”.
“Baadhi ya shule zitakzofaidika na mpango huu ni pamoja na shule ya
Msingi Pongwe Tanga itakayojengewa darasa, shule ya msingi ya
kumbukumbu Dar es salaam itapatiwa msaada wa viti na meza kwa darasa
la watoto wa masomo ya awali, shule ya sekondari Ndala watapewa vifaa
vya ofisi kwa wafanyakazi , uhuru mchanganyiko watanunuliwa mashine
ya Braile pamoja na vifaa vya kufundishai na shule ya msingi kimara
watapatiwa tanki ya kuhifadhi maji.
Nia yetu ni kuhakikisha tunazifikia shule nyingi zaidi na jamii kwa
ujumla “aliongeza Mmbando.Airtel Tanzania imekuwa mstari wa mbele
katika kusaidia sekta ya elimu nchini mpaka sasa zaidi ya shule 1000
zimeweza kufaidika na vitabu kupitia mradi wa Shule yetu” wiki
iliyopita
Airtel imetangaza zaidi ya shule 30 zitakazofaidika na misaada ya
vitabu kwa mwaka huu wa 2014 na leo kupitia wafanyakazi wake Airtel
inaendelea kuwafikia watu wengi zaida na jamii nzima kwa ujumla nchini
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...