Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasalimia wakazi wa Kibaha mjini wakati wakiwasili kwenye uwanja wa mkutano .
 Kikundi cha ngoma cha Kisamamwe kikitumbuiza ngoma ya Afrika kabla ya kuanza kwa mkutano wa hadhara ambapo Katibu Mkuu wa CCM alihutubia wananchi wa Kibaha mjini.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kibaha mjini ambapo aliwaambia wapinzani wamekosa hoja ya msingi kiasi cha kuamua kufanya maandamano ya kuleta vurugu nchini.
 Sehemu ya Umati wa watu wakisikiliza mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wana CCM wakiwa kwenye mkutano
 Mbunge wa Kibaha mjini Silvestry Francis Koka akihutubia wakazi wake na kuwaambia kuwa pamoja na jitihada zote anazofanya maji bado ni donda sugu ila ufumbuzi upo njiani.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kibaha mjini wakati wa mkutano wa hadhara ambapo aliwaambia viongozi wa halmashauri hawana budi kukaa na wafanya biashara ndogo ndogo kujadili kodi kabla ya kuwapangia kuona kama wana uwezo wa kulipa ama hapana hii itasaidia kupunguza lawama na mikingamo baina ya wafanya biashara na halmashauri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...