Dotto Mwaibale
TAASISI ya sanaa na utamaduni Bagamoyo (TaSUba) imeanadaa tamasha la 33 lenye lengo la kukuza mila na desturi za watanzania.
Katika
tamasha hilo kauli mbiu itakuwa sanaa na utamaduni katika kukuza utalii
na mgeni rasmi ni Mbunge wa Afrika Mashariki Makongoro Nyerere ambaye
atamwakilisha Spika wa Bunge la Afrika Mashariki, Spika wa Bunge hilo
Margareth Zziwa .
Akizungumza Dar es Salaam, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUba), Michael Kadinde alisema tamasha hilo pia lina lengo la kuonyesha sanaa zilizoandaliwa kiutalaam na wanafunzi wa Tasuba.
"Katika
tamasha hili pia tuaihamasisha jamii ije ione tofauti ya sanaa
iliondaliwa kitaalamu na isiyo kitaalamu kuweka ushindani kati kati ya
taasisi yetu na vikundi vingine,"alisema.
Kadinde alisema katika taasisi yao wanafundisha maigizo,ngoma muziki ufundi wa majukwaa,sanaaza ufundina filamu za televisheni.
"Vikundi
ambvyo vitashiriki katika tamasha hilo vya ndani ni 143 na vikundi vya
nje vitakuwa vitano Kenya watakuwa na fani ya ngoma,Newzealand watakuwa
na muziki, Norway, watakuwa na muziki,Newzealand muziki,Ujerumani
maigizo na ,na Korea Kusini watakuwa na muziki,"alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...