BAADHI ya wanachama wa mfuko wa Bima ya afya (NHIF) wameutaka mfuko huo kugharamia kipimo cha vina saba (DNA) kwa wananchama wake pamoja na gharama za nauli na posho kwa wanachama wanaokwenda kupata matibabu nje ya vituo vyao vya kazi.

Wanachama hao waliyasema hayo katika kijiji cha Mwamgongo wakati wa kikao cha pamoja baina ya wanachama hao na uongozi wa mfuko wa Bima ya afya(NHIF) Mkoa wa Kigoma.

Nassib Ally mtumishi wa afya katika kituo cha mwamgongo alisema kuwa pamoja na kwamba malipo ya posho na nauli kwasasa ya kwenda kutibiwa nje ya kituo hulipwa na mwajiri lakini malipo hayo hayalipwi kwa wakati.

Alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikiwafanya wanachama kuhangaika wanapofuatilia matibabu nje ya vituo vyao vya kazi.

Naye Mussa mwalimu wa shule ya Msingi Nyambusho iliyopo kijijini hapo alisema kuwa aliutaka mfuko kugharamia upimaji wa vinasaba(DNA)pamoja na kugharamia matibabu ya nje ya nchi kwa wananchama wake.

Akijibu juu ya maombi hayo Meneja wa Bima ya afya Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo alisema kuwa kwasasa mfuko wa Bima ya afya haugharamii malipo ya posho na nauli kwa wanachama wake wanaopata rufaa ya matibabu nje ya vituo vyao vya kazi,Alisema suala hilo linabaki kuwa la muajiri.

Odhiambo alisema pia suala la kugharamia matibabu nje ya nchi litabaki suala la Wizara ya afya na huku suala la upimaji wa vinasaba likibaki kuwa la gharama za mtu binafsi.
Meneja wa mfuko wa Bima ya afya (NHIF)Mkoa waKigoma Elias Odhiambo akikabidhi moja ya mashuka 50 kwa uongozi wa Kituo cha afya cha Mwamgongo kilichopo mwambao wa kaskazini mwa Ziwa Tanganyika Wilaya ya Kigoma.
Mkuu wa kituo cha afya Mwamgongo Dkt Swagala akipokea msaada wa mashuka 50 toka kwa meneja wa Bima ya afya(NHIF)Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha mwamgongo waliojitokeza kupima afya zao katika shule ya msingi mwamgongo zoezi lililokuwa likiratibiwa na mfuko wa Bima ya afya(NHIF) Mkoa wa Kigoma.Picha zote na Editha Karlo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...