Akiwa ziarani Ethiopia Waziri  wa Nchi (Kazi Maalum) Ofisi ya Rais, Profesa Mark Mwandosya Mwandosya ametembelea mradi wa ujenzi wa Bwawa Kuu la Ethiopia (Great Ethiopian Renaissance Dam-GERD).Ujenzi utakapokamilika mwaka 2017 GERD litazalisha MW 6000 za umeme na kuwa mradi mkubwa wa aina yake Afrika na wa nane kwa ukubwa duniani. Mradi unahusu ujenzi wa bwawa kwenye Mto Blue Nile, kilomita 850 kutoka Addis Ababa.
Waziri  wa Nchi (Kazi Maalum) Ofisi ya Rais, Profesa Mark Mwandosya Mwandosya na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe. Naimi Aziz (wa pili kushoto) wakitembelea mradi wa ujenzi wa Bwawa Kuu la Ethiopia (Great Ethiopian Renaissance Dam-GERD).
Waziri wa Maji Umwagiliaji na Umeme wa Ethiopia Mheshimiwa Alemayehu Tegenu,kushoto,na Waziri wa Nchi (Kazi Maalum)Ofisi ya Rais,Mark Mwandosya ,kulia,wakipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Mradi Mhandisi Bekele. 
Waziri Tegenu wa Ethiopia akiwa katikati mwenye kofia ya kijani,kulia kwake ni Mheshimiwa Naimi Aziz,Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, wa kwanza kushoto kwake ni Mama Lucy Mwandosya,mke wa Waziri Mwandosya, wa pili kushoto kwake ni Waziri Mwandosya,wa tatu kushoto kwake ni Mhandisi Bekele,Meneja wa Mradi,wakiwa na wahandisi wa mradi, na ujumbe wa Waziri Mwandosya. 
Eneo la Mradi wa ujenzi wa Bwawa Kuu la Ethiopia (Great Ethiopian Renaissance Dam-GERD)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Wakati huu kuna maendeleo ya kasi yanayoendelea ikiwemo kujenga miundo mbinu Ethiopia

    ReplyDelete
  2. Mwandosya Rais 2015

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...