Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini Jumatatu ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete asubuhi ya Jumatatu, Desemba 22, 2014, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa
Afrika Kusini, Mheshimiwa Jacob Zuma.
Mazungumzo
hayo yaliyofanyika Ikulu, Dar Es Salaam, yalichukua kiasi cha saa moja na
dakika 45 na yalihusu uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini.
Rais
Zuma ambaye aliwasili nchini usiku wa jana, Jumapili, Desemba 21, 2014,
ameondoka nchini mara baada ya kumalizika mazungumzo hayo.
Imetolewa
na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
22 Desemba,
2014
Zuma you are looking sharp Mr President in that bright coloured suit!!
ReplyDelete