Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais,Mhe Ummy Mwalimu kupitia Taasisi ya Maendeleo ya Wanawake wa Mkoa wa Tanga (TAWODE)
ameendesha mafunzo ya kuwajengea uwezo wasichana wa Wilaya ya Muheza, Mkoani Tanga
wenye umri kati ya miaka 10 - 24. Lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha wasichana hao
kujitambua na kujithamini katika masuala ya afya ya uzazi ili kujikinga na mimba na ndoa za
utotoni na maambukizi ya VVU/UKIMWI.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais,Mhe Ummy Mwalimu akifungua mafunzo kwa wasichana wa Wilaya ya Muheza juu ya kujitambua
na kujithamini katika masuala ya Afya ya uzazi. Mafunzo hayo yamefanyika mwishoni mwa
wiki Wilayani Muheza.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais,Mhe Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya kujitambua na kujithamini Wilayani Muheza mwishoni mwa wiki.
Wasichana wa Wilaya ya Muheza wakifanya majadiliano na mawasilisho katika vikundi juu ya
changamoto wanazokumbana nazo katika kipindi cha ujana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...