Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii

KIKOSI cha polisi usalama barabarani kimewataka madereva wa mabasi ,magari makubwa pamoja na daladala kwenda kusoma ili kuongeza ujuzi wa kazi zao kutokana na kuwepo kwa teknolojia za kisasa katika magari hayo.

Hayo ameyasema,Ofisa Mnadhimu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Johansen Kahatano wakati wa semina ya kuwajengea uwezo madereva katika kukabiliana na ajali za barabarani iliyofanyika jana katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.

Alisema sheria ya madeva wa mabasi ya abiria na magari makubwa kwenda kujiendeleza kimasomo pamoja na kupata ujuzi  kwa kila baada ya miaka miwili pamoja na kupewa leseni mpya  kwa sababu leseni zote zinakaribia kuisha muda wake.

Kahatano, alisema kuwa madereva wote wa malori wanatakiwa kusoma, kujikumbushia vitu mbalimbali na kuongeza ujuzi wao kwa kila baada ya miaka 3, ilikupunguza ajari za barabarani.

Katika semina hiyo waendesha daladala wamesema kuwa kama serikali imeamua madereva twende darasani tena,  tunaomba gharama zote za mafuzo hayo ziwe za waajili wetu au serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Naunga mkono warudi kabisa inaweza kusaidia kupunguza ajali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...