Na John Nditi, Morogoro

MKUU  wa wilaya ya Mvomero, mkoa wa Morogoro, Festo Kiswaga, Machi 31, 2015,  amefungua mkutano wa siku mbili wa Baraza la wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania, unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli Oasis , mjini Morogoro.

Mkuu huyo wa wilaya alimwakilisha mkuu wa mkoa, Dk Rajab Rutengwe ,na  katika hotuba yake ya ufunguzi wa Baraza hilo ,amewapongeza wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kwa kuendeleza na kuitangaza taaluma yao vizuri ya utabiri wa  hali ya hewa ikiwa na  kuelimisha umma wa watanzania.

Pamoja na hayo alisema , Mamkala hiyo  imekuwa mstari wa mbele kutoa taarifa za hali ya hewa zitolewazo kila siku, siku kumi na zile za msimu pamoja na tahadhari kutokana na hali mbaya ya hewa , kutokana na hali hiyo TMA imeendelea kuaminika katika macho ya mii ya watanzania na kuweza kuchangia kuinua uchumi wa nchi yetu.

Kwa upande wake , Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi, mbali na kuelezea changamoto kubwa ya ufinyu wa bajeti, amesema kuwa , wataendelea kutoa tabiri wa kila siku ambao ni muhimu kwa wananchi na wakulima kuutumia katika kilimo ili kupata mazao mengi yenye kuwaletea tija .

Alisema , utabiri huo inaonesha mifumo ya hali ya hewa na kutokea kwa mvua na kukosekana kwa mvua za kutosha , hali inayowawezesha kutumia muda mupi wa hali ya hewa na mvua kupanda mazao ambayo nayakomaa kwa muda mfupi na kuvuna mazao mengi, ambapo pia amewataka maofiza ugani kusambaza matokeo ya utabiri kwa wakulima vijijini .
Mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Mvomero, Festo Kiswaga akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Kijazi katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi ( kulia) akinukuu jambo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi DC wa Mvomero (kati kati), Festo Kiswaga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...