Na DORICE Kigombe wa Jeshi la Polisi Dodoma.

Jeshi la Polisi Mkoani Dodoma kwa kushirikiana na Idara mbalimbali za Serikali na wadau wa Amani Raia ,wamefanya matembezi/Routmatch ya pamoja kuzunguka mitaa mbalimbali ya mji wa Dodoma .Matembezi yaliongozwa na Mkuu wa Mkoa Dodoma Capt. Mstaafu CHIKU GALAWA.

Washiriki wa zoezi hilo ni Jeshi la Polisi, Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jeshi la Magereza, Uhamiaji, Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Wafanya biashara, Raia wema na watumishi raia wa Vyombo vya ulinzi na Usalama Mkoani Dodoma.

Lengo la zoezi hili la pamoja ni kudumisha ushirikiano, mahusiano mema ya idara mbalimmbali za serikali na raia wema. Akiongea na washiriki wa zoezi hilo, Mh. Mkuu wa Mkoa Capt. Mstaafu CHIKU GALAWA alisema “mazoezi ni afya, ushirikiano ni furaha na kukuza Udugu. Aliwapongeza wote walioshiriki zoezi hilo na kuagiza kuwa litakuwa zoezi endelevu na litashirikisha Idara nyingi zaidi.
Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na usalama Mkoa wa Dodoma,  Mkuu wa Mkoa Dodoma Capt. Mstaafu Chiku Galawa akiwa na wajumbe wakuu katika Routmatch leo.

Askari polisi wa Mkoa wa Dodoma wakiwa katika Routmatch leo.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Capt. Mstaafu Chiku Galawa akizungumza na washiriki wa Routmatch baada ya kuhitimisha zoezi katika viwanja vya bwalo la Polisi Dodoma leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...