Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anna Makinda akiwa katika Mkutano wa Kumi wa Maspika Wanawake uliofanyika kwa siku mbili hapa Umoja wa Mataifa, Mkutano wa Maspika Wanawake, umetangulia Mkutano wa Nne wa Maspika zaidi ya 180 unaoza leo jumatatu hapa Umoja wa Mataifa.
Sehemu ya Wajumbe wa Mkutano wa Kumi wa Maspika wanawake, mkutano uliojadili mbinu za kuchagiza usawa wa kijinsia, miaka 20 baada ya Beijing pamoja na kuhakikisha utekelezaji wa malengo 17 ya Maendeleo Endelevu Baada ya 2015.
Maspika Wanawake wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa IPU Bw. Choedhury Saber na Katibu Mkuu wa IPU Bw. Martin Chungong wakati wa mkutano wao wa siku mbili uliofanyika jumamosi na jumapili, ukitangulia mkutano wa nne wa Maspika wa Mabunge.
Na Mwandishi Maalum, New York
MKUTANO wa Nne unaowakutanisha
Maspika 180 na Manaibu Spika 35 kutoka
nchi 140, unaanza leo ( jumatatu) hapa
Makao Mkuu ya Umoja wa Mataifa.
Mkutano huu wa siku tatu na
ambao umeandaliwa na
Chama cha Mabunge Duniani ( IPU), utafunguliwa na Rais wa IPU
Bw. Chowdhury Saber na Katibu Mkuu wa Umoja wa Matafa, Ban Ki Moon.
Spika wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Ann
Makinda anaongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano huu.
Mkutano ambao
Maspika wanatarajiwa kujadiliana kwa kina namna ya kukabiliana na
changamoto za Amani, Demokrasia na Maendeleo kwa maono ya Kibunge.
Mkutano wa Nne wa Maspika,
ulitanguliwa na Mkutano wa
Kumi wa
Maspika wanawake, mkutano uliofanyika kwa siku mbili ( jumamosi na
Jumapili). Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Ann Makinda ameshiriki kikamilifu na kuongoza baadhi ya mikutano.
Mkutano wa Nne wa Maspika
ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya
Maspika hao na ambayo imekuwa ikifanyika kuelekea Mkutano wa Kilele wa
Viongozi wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika wiki chache zijazo ambapo
watapokea na kupitisha Ajenda Mpya
za Maendeleo Endelevu baada ya 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...