Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma(kushoto) akikabidhi jezi kwa kapteni wa timu ya G Unity Fc kwa ajili ya mchezo wa fainali uliofanyika katika kiwanja cha Kipunguni B katika kata ya Kipunguni manispaa ya Ilala jijini Dar. Ambapo timu ya G Unity FC waliibuka washindi baada ya kuichapa timu ya Sukuma Land Fc bao 5 kwa 2.
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Eliaichi Remmy(kushoto) akitoa somo kwa madereva bodaboda kuhusu Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa Hiari(PSS) waliofika katika mchezo wa fainali katika uwanja wa Kipunguni B
Mmoja wa Madereva Bodaboda akisoma maelekezo ya jinsi ya kutuma pesa kwenye akaunti kwenye mfuko wa Uchangiaji wa Hiari(PSS) mara baada ya kupatiwa kitambulisho cha uanachama wa mfuko wa PSPF.
 
Maafisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF wakiwa kwenye picha ya pamoja na waratibu wa michezo hiyo pamoja na Timu ya G Unity Fc walioibuka washindi wa wa kwanza baada ya kufunga timu ya Sukuma Land Fc mabao 5 -2, mchezo huo uliofanyika katika kiwanja cha Kipunguni B
Mbwembwe za mashabiki katika fainali hizo
Mkurugenzi mtendaji wa kata ya Kipunguni na Kivule Dr. Kadry Pinde ambaye alikuwa ni Mgeni rasmi katika mchezo wa fainali akikabidhi mpira kwa kapteni wa timu ya Kilimani Fc walioibuka washindi wa wa nne katika mashindano ya mpira wa miguu kwa madereva Bodaboda wa kata ya Kipunguni. Wa kwanza kushoto ni Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Ismail Juma.

Mashabiki wakiendelea kufuatia kinachijili uwanjani

MASHINDANO ya ligi wa mpira wa miguu kwa madereva bodaboda yahitimishwa na wadhamini wa mashindano hayo ambao ni mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa kuweza kuwasajiri wachezaji katoka mfuko wa hiari wa PSS. Ligi hiyo iliyodumu ndani ya siku saba (7) ambapo alikuwa akitafutwa mshindi atakayeweza kuwa balozi mzuri wa mfuko wa penshenI wa PSPF yamemalizika kwa timu 32 kumenyana vikali na timu  ya G Unity kuibuka kinara ambapo timu hiyo ndiyo iliyotawazwa na kuwa balozi wa PSPF katika kata ya Kipunguni  mara baada ya fainali iliyohusisha timu ya Sukuma Land FC na G Unity Fc na hatimaye timu yaG Unity kuibuka kinara kwa bao 5 kwa2 katika fainali iliyopigwa katika kiwanja cha Kipunguni B.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...