Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sophia Mjema (katikati) kabla ya kuanza zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
Petra Karamagi na Nasser Ngenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa wakishikishiriki zoezi la usafi katika soko la Temeke Stereo.
Zoe Glorious katika ubora wake.
#HapaKaziTu ......Usia Nkhoma Ledama akiwajibika katika zoezi la usafi soko la Temeke Stereo.
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu (kulia) akiteta jambo na na baadhi ya maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walioshiriki kwenye zoezi la kufanya usafi wa mazingira katika soko la Temeke Stereo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...