Imeelezwa kwamba licha ya serikali kuendelea kutoa kipaumbele katika sekta ya elimu bado sekta hiyo imeendelea kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa miundombinu. https://youtu.be/nYm0I2QUYNs
Wakati manispaa ya Kinondoni ikifanya jitihada za ujenzi wa shule za sekondari ili kuwanusuru wanafunzi waliofaulu na kukosa shule wilayani humo, changamoto ya walimu wa hisabati na sayansi yaendelea kujitokeza.https://youtu.be/A6ZFwZQwaCE
Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma latengua uamuzi wake wa kulifukuza shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masuala ya uboreshaji wa sekta ya afya la SIKIKA.https://youtu.be/pXyKSCJIR78
Wachimbaji wadogo mkoani Geita wailalamikia ofisi ya madini ya mkoa huo kwa madai ya kuwatimua kwenye eneo la madini waliloligundua siku kadhaa zilizopita huku wakiwasilisha kilio chao kwa waziri mwenye dhamana.https://youtu.be/3L5G_GI4WHY
Imeelezwa kwamba mikakati ya kukabiliana na matatizo ya macho haitafanikiwa endapo wananchi wenyewe hawatawahi kupata matibabu mapema ili kuzuia upofu utotoni hadi uzeeni. https://youtu.be/7GTQ33OHYHQ
Rais John Magufuli awataka wamiliki wa mashamba na viwanda vilivyotelekezwa kuviendeleza kabla ya hatua kali kuchukuliwa dhidi yao;https://youtu.be/gRoVPtGQYu0
Serikali yasema itadhibiti matumizi yasiyo ya lazima ili kusimamia vilivyo fedha za umma katika matumizi yaliyokusudiwa; https://youtu.be/z1vfSCMiM-M
Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata magari mawili yalihusika na wizi katika ofisi ya kamishina wa TRA;https://youtu.be/DW9Vanzv6qY
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt Jakaya Kikwete awataka wazee mkoani Singida kuunga juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano;https://youtu.be/XQ6MgRBjVRE
Wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiliano yataja gharama zilizotumika katika ununuzi wa mabehewa 274 ya mamlaka ya reli nchini TRL;https://youtu.be/jvbjeliDXig
Mkuu wa wilaya ya Monduli, Mhe. Francis Miti aamuru kuwekwa ndani kwa maafisa wanne wa idara ya ardhi kwa tuhuma ya ubadhlifu wa fedha za umma;https://youtu.be/5Q2fNVhqzJY
Wakulima wilayani Makete waiomba serikali kutazama upya bei ya zao la Pareto ili mkulima aweze kunufaika na zao hilo; https://youtu.be/DmNtToiwvjI
Serikali yashauriwa kuzingatiwa suala la mabadiliko ya tabia nchi katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo ya barabara na kilimo; https://youtu.be/lb95LitE0Fk
Jeshi la polisi kanda ya maalum ya Dar es Salaam yapiga marufuku kwa madereva wa bodaboda kufanya biashara hiyo bila ya kuwa na leseni;https://youtu.be/wI0Yi3Y3i1Q
Timu ya Azam yajitapa kufanya vizuri katika michezo ya ligi kuu soka Tanzania Bara; https://youtu.be/JiDQDNV6l4A
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...