NA EVELYN MKOKOI

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano za Mazingira Mhe. Luhaga Mpina ameshiriki usafi wa mazingira wa kila jumamosi ya mwisho wa mwezi, mara hii mkoani Simiyu katika wilaya ya Meatu jimboni Kisesa.

Akizungumza na wananchi wa eneo la Mwandoya wilayani Meatu, Mhe. Mpina amewaasa wananchi wa mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuitunza miti 4820 iliyopokelewa na kupandwa wilayani hapo baada ya serikali ya awamu ya tano kutekeleza ahadi yake ya kuupatia Mkoa wa Simiyu idadi hiyo ya miti.

Naibu Waziri Mpina, alisema kuwa kwa kuwamkoa wa simiyu huko kwenye hatari kubwa ya kuwa janga na umesha wahi kukabiliwa na tatizo la uhaba wa chakula, kabla ya uchaguzi uliopita, kwa kuitunza miti hiyo ya matunda wakazi wa mkoa huo watanufaika na miti ya matunda hayo ya muda mfupi kwa kufanya biashara ili kuweza kukuza uchumi na kuongeza kipato cha kila mmoja.
Aliongeza kuwa, zoezi la upandaji miti mkoani simiyu katika ma shule, maeneo ya makazi ya watu na mashamba yanahitaji utunzani mkubwa kwani miti hiyo ina uwezo mkubwa wa kuboresha uoto wa asili ambao mpaka hivi sasa umetoweka.

Aidha Mhe. Mpina amewataka viongozi wa mkoa wa Simiyu kuchukua nafasi yao kusimamia wanachi wafanye usafi ikiwa ni agizo la serikali la kila mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi na kuwa viongozi ambao watakuwa wazembe katika suala zima la usimamiaji wa usafi wa mazingira watachukuliwa hatua.

Alipoongea na wanachi wa Jimbo La Kisesa, Naibu Waziri Mpina aliwaasa wananchi wa Kisesa wa sapoti jitihada za serikali za kupanda miti na kutunza mazingira, na kuwa hakikishia wapiga kura wake kuwa pamoja na kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, nafasi za kazi yake kama Mbunge wa jimbo hilo ipo pale pale na ataendelea kuwapigania wana Kisesa.

Aliwaomba wana Kisesa wawe mfano wa kupanda miti iliyotolewa na serikali na kuitunza na kwa aliokosa miche ya miti hiyo iliyogawiwa ame ahidi kuwapatia miche mingine kwani shabaya yake kubwa ni kuwezesha mkoa wa simiyu kupata miti hasa ya matunza na mbao ili kuboresha uchumi binafsi na pato la taifa.

Mhe. Mpina Amefanya usafi wa mazingira leo katika eneo la hospital ya Mwandoya pamoja na kupanda miti ikiwa ni sehemu ya utekekezaji wa kampeni ya kitaifa ya kupanda miti.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 02, 2016

    Hawa wanafyeka pori au kufanya usafi maana picha iliyobandikwa inatatanisha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...