kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa anaonyeshwa moja ya miradi ya UVCCM wilaya ya Same.
Na Woinde Shizza, Same
Wabunge wa upinzani wametakiwa kuwatetea wananchi, kutatua kero zao pamoja na kuwawakilisha vyema wanapokuwa bungeni na sio kufanya kazi ya kutoka nje ya bunge kwa mambo ya siyokuwa ya msingi.
Hayo yamebainishwa leo na kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka wakati akiongea na wananchi wa wilaya ya Same katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa standi ya Same.
Alisema kuwa ni jambo la kuchekesha na kushangaza kuona kiongozi ambaye amechaguliwa na mwananchi ili akamuwakilishe kwa kupeleka kero zao bungeni anafika bungeni na kutoka nje kutokana na sababu zisizo za msingi.
"unajua ni jambo la kushangaza kuona mbunge anasusia kikao cha bunge kisa eti serekali imekata a kurusha vikao vya bunge live sasa jamani uyu mbunge katumwa kuuza sura kwenye televisheni au kupeleka kero za wananchi, mbona awa Wabunge watakuwa kama harusi iliyokosa Vyombo "alisema shaka
Alibainisha kuwa wananchi wa nataka kutekelezewa ahadi zao na sio kuona sura zao kwenye tv, na kuaidiwa ahadi zisizo tekelezwa.
Alisema kuwa wananchi wa sasa hivi wanataka maendeleo, na viongozi kuona Sura zao bungeni wakiwa wanafanya mambo ya ajabu na ya kutia aibu wanapokuwa bungeni.
Aliongeza kuwa iwapo kama viongozi wa upinzani wameshidwa kufanya kazi waliotumwa na wananchi wao basi waachie ngazi kwa kujiuzuru ili waweza kufanya kazi na wanaotambua nini wajibu wao bungeni.
Aidha Alibainisha kuwa viongozi wa CCM pamoja na serekali wamejipanga vyema kuhakikisha wanatatua kero za wananchi na kuwatimizia yale yote ambayo waliahidi kwa wananchi wakati wa kipindi cha kampeni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...