SHIRIKISHO la Soka barani Africa (CAF) limepata mdhamini mpya baada ya kumalizika kwa mkataba wake na kampuni ya mawasiliano ya Orange.

Orange imekuwa mdhamini mkuu wa mashindano makubwa ya CAF kwa miaka minane tangu 2009.

Kabla ya hapo, kampuni nyingine ya mawasiliano ya MTN ndiyo iliyokuwa mdhamini kwa miaka minne.
Sasa, mdhamini mpya atakuwa kampuni ya mafuta na gesi ya Total kutoka Ufaransa.

Kampuni hiyo itaanza kwa kudhamini michuano ya Kombe la Taifa Bingwa Afrika mwaka 2017 ambayo itaandaliwa nchini Gabon. Thamani ya mkataba huo haijafichuliwa.

Total itakuwa mdhamini mkuu wa:
Kombe la Taifa Bingwa Afrika
Ligi ya Klabu Bingwa Afrika
Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN)
Super Cup ya Afrika
Kombe la Mashirikisho
Kombe la Taifa Bingwa Afrika kwa Wanawake
Kombe la Futsal Afrika
Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 23
Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 20
Kombe la Taifa Bingwa Afrika wachezaji wa chini ya miaka 17.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...