Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kikazi katika Hospitali ya Rufaa ya Maweni ya Mkoa wa Kigoma na kujionea mambo mbalimbali.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri aliweza kubaini mapungufu kadhaa ambapo amewataka uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha wanatatua matatizo hayo haraka. Miongoni mwa matatizo hayo ni pamoja na kutokuwa na mfumo maalum wa kukusanya mapato kwa njia ya kielektroniki ili kudhibiti mapato huku akiwataka ndani ya miezi mitatu wawe wameshakamilisha mfumo huo.

Mbali na hilo pia amewataka kuzingatia utunzaji wa vifaa vya Maabara ya Hospitali hiyo kwani licha ya kuwa na jingo zuri lakini bado hali ya utunzaji imekuwa ndogo na hata kusababisha vifaa vingine havifanyi kazi.

Kwa upande wa Chumba cha upasuaji (Theatre) amewaagiza kuhakikisha wanaondoa kasoro zote muhimu kwani Chumba hicho kimekosa sifa ya kuitwa Chumba cha Upasuaji cha Hospitali ya Mkoa wa Kigoma baada ya kushuhudia ufinyu wa jengo lenyewe, ukosefu wa vifaa na hali nzima ya sehemu ya utendeaji kazi.

Naibu Waziri wa Afya ametembelea Mkoa Kigoma katika ziara yake ya siku mbili, awali aliweza kutembelea Kituo cha Afya cha Uvinza kilichopo Wilaya ya Uvinza, pamoja na Hospitali ya Heri Mission iliyopo Wilayani Buhigwa Mkoani humo.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akipatiwa maelezo kutoka kwa msimamizi wa Maabara ya Hospitali ya Mkoa wa Kigoma.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maelezo ya maboresho.
Baadhi ya Madaktari na wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla (Hayupo pichani) alipokuwa akizungumza nao na kupata maoni yao juu ya utendaji kazi Hospitali hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...