Na Nteghenjwa Hosseah, ARUSHA 

SERIKALI imesema kuwa inaanza kufanya maboresho kwa kuandaa na kuhakikisha Sera ya Uboreshaji wa Viwanda vya Dawa vilivyopo nchini kwa kuwawezesha na kuwajengea uwezo wenye viwanda nchini ili waweze kuzalisha dawa na kupunguza uagizaji wa dawa kutoka nje ya nchi.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo kwa niaba ya Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza katika Kongamano la 49 la Chama Cha Wafamasia Tanzania (PST),linalofanyika jijini hapa kwa siku mbili.

Akizungumza kwa niaba ya Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,alisema kuwa kutokana na umuhimu wa sekta hiyo ya dawa, Serikali inaangalia taaluma hiyo kwa macho mawili kwa lengo la kuiboresha ili iweze kutoa huduma bora.

"Wizara yangu inaangalia taaluma hii kwa macho mawili katika kuhakikisha kuwa sekta ya dawa inaboreka na inakua na hatimaye kuweza kukuza uchumi wetu, kwa kuwawezesha na kuwajengea uwezo wenye viwanda nchini ili waweze kuzalisha zaidi ikiwa ni pamoja na kuwahakikishia soko ndani ya nchi na kupunguza uagizaji wa dawa kutoka nje ya nchi na hivyo kuwa na dawa bora, salama na zenye ufanisi"

"Endapo tutazalisha dawa zetu wenyewe hii itatupunguzia gharama zisizo za lazima kuagiza dawa nje ya nchi, sambamba na hili pia tunaboresha vyuo vya Wafamasia ili waweze kutoka wataalamu bora wa masuala haya ya madawa,”alisema Gambo

Akizungumzia suala la wizi wa dawa katika hospitali za serikali,alisema kuwa Serikali haina mchezo na yoyote atakayokiuka maadili ya taaluma hiyo na kuwa watawachukulia hatua kali za kisheria ili wananchi wapate huduma bora za dawa. "Mbali na changamoto ya upungufu wa dawa, wafanyakazi wasio waadilifu ambao wanatumia nafasi zao vibaya wanashirikiana na baadhi ya wafanyabiashara na kuuza dawa, hili ni suala muhimu PST jadilianeni suala la maadili kwani hatua za kisheria dhidi yao zitachukuliwa"alisema

Awali Rais wa PST, Michael Kishiwa, aliiomba Serikali kuongeza udahili wa wanafunzi wa famasia wakiwemo mafamasia wasaidizi ili kutoa dawa sahihi kwa wagonjwa. Alisema hivi sasa idadi ya watanzania ni kubwa, lakini wataalamu wa dawa Wafamasia ni 1,200, hali inayochangia kuwepo kwa watoa huduma hiyo wasio na sifa. Alisema kutokana na kukosekana wanataaluma kumekuwepo na changamoto kubwa ya baadhi yao kukiuka maadili na wengine kufanya kazi ya utoaji dawa pasipokuwa na uelewa nayo, hali ambayo hatari kwa afya za binadamu.

Kishiwa alisema kazi kubwa ya chama chao kuhakikisha inasimamia ubora wa utoaji huduma ya dawa na kusimamia maadili, ili wananchi wapate dawa sahihi na kuzitumia ipasavyo. “Tunashirikiana na baraza la usajili la wafamasia katika kukemea vitendo hivyo vya ukiukwaji wa maadili na ndiyo maana tunaiomba serikali iongeze udahili na vyuo vinavyotoa taaluma hii"alisema

Naye Msajili wa Baraza la Wafamasia, Elizabeth Shekalage alisema kwa sasa wananchi wengi wamechukulia huduma ya dawa ni biashara na kuwa baraza limejipanga kupambana na watu wanaofanya huduma hiyo ni biashara huku wakikiuka maadili.

"Uchache wa wanataaluma unasababisha kika mtu aone hii ni biashara huria na yeyote anaweza kuifanya,kuna uhaba mkubwa wa fundi dawa sanifu,mafundi dawa wasaidizi,dawa ni sumu hivyo tunasimamia hili ili kuepusha madhara kwa watumiaji"alisema Elizabeth

Kongamano la Mwaka huu linaenda na kauli mbiu isemayo kuelezea ubora,usalama,ufanisi na upatikanaji wa huduma bora za kifamasia.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo akitoa hotuba katika ufunguzi wa kongamano la 49 la Chama cha Wafamasia Tanzania.

Rais wa Chama cha wafamasia Tanzania (PST) Ndg. Michael Kishiwa (aliyesimama)akitoa taarifa ya Chama kwa kifupi kwa Mgeni Rasmi Mhe. Mrisho Gambo katika Kongamano la 49 la wafamasia Tanzania linalofanyika Jijini Arusha.
Wanachama wa PST wakifuatilia ufunguzi wa Kongamano .
 

Wajumbe wa kongamano wakiendelea kufuatilia Hotuba ya Ufunguzi .
1. Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo(Kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na dawa Hiti Silo katika Kongamano la  wafamasia linalofanyika katika Jiji la Arusha. 
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...