Zuena Msuya, Mtwara

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali Madini (SMMRP) ulio chini ya Wizara ya Nishati na Madini, umekabidhi Jengo la kisasa kwa Kanda ya Madini Kusini ambalo linatarajiwa kurahasisha utendaji kazi kwa kutumia mfumo wa teknolojia ya kisasa.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi jengo hilo mkoani Mtwara hivi karibuni, Msanifu Majengo wa SMMRP, Joseph Ringo alisema kuwa, ujenzi wa jengo hilo umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia mradi huo kwa lengo la kuboresha Sekta ya Madini nchini.

Ringo alisema kuwa, jengo hilo ambalo litatumika kama kituo cha Kisasa cha Madini (Center for Excellence) limeunganishwa katika mfumo wa kisasa wa TEHAMA kwa kuhifadhi taarifa pamoja na kumbukumbu mbalimbali za kidijitali za madini za Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake na endapo itatokea tatizo katika mfumo huo itakuwa ni rahisi kupatikana.

Alifafanua kuwa, jengo hilo limeunganishwa na mfumo wa kisasa wa TEHAMA, Ofisi za watendaji wa wizara, maktaba ya kisasa ya kuhifadhia taarifa za madini yanayopatikana katika ukanda wa kusini pamoja na uwepo wa vyumba maalumu vyenye vifaa kwa ajili ya kutolea mafunzo kwa wachimbaji wa madini.

Aidha, Ringo alifafanua kuwa, mradi wa SMMRP umelenga katika kuboresha miundombinu hasa ya majengo kwa kuweka mifumo ya kisasa pamoja na kuimarisha shughuli za rasilimali madini katika Ofisi za Kanda na Mikoa nchini.

Kwa upande wake, Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka alisema kuwa hivi sasa jengo hilo litawasaidia kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi kwakuwa lina uwezo wa kukidhi miundombinu yote ya wafanyakazi. Vilevile, amewataka wafanyakazi watakaokuwa wakitumia jengo hilo kuitunza na kulinda miundombinu ya jengo hilo.

Jengo hilo limebuniwa na Kampuni ya OGM Architects Consultants na kujengwa na kampuni ya ukandarasi ya Malcom Investment Co Ltd.

Mwakilishi wa kampuni ya ukandarasi ya Malcom Investment Co Ltd (mwenye tshirt ya bluu) waliojenga jengo hilo, akikabidhi ufunguo kwa Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali watu wa Wizara ya Nishati na Madini Bibi Joyceline Lugora (katikati) wakati wa kukabidhi jengo hilo kwa kanda ya madini kusini mkoani Mtwara hivi karibuni.
Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (aliyeshika ufunguo) baada ya kupokea kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali watu wa Wizara ya Nishati na Madini, Joyceline Lugora (katikati) tayari kuanza kulitumia jengo hilo kabla ya kuzinduliwa rasmi hivi karibuni.
Taswira ya muonekano wa upande wa kulia wa jengo hilo la Ofisi ya Madini Kanda ya Kusini mkoani Mtwara. 
Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Mhandisi Benjamin Mchwampaka,(kulia) na Mkurugenzi Msaidizi Rasilimali watu wa Wizara ya Nishati na Madini Joyceline Lugora wakitia sahihi nyaraka za kukabidhiwa jengo la Ofisi ya Madini Kanda ya Kusini mkoani Mtwara wakishuhudiwa na  Msanifu Majengo wa SMMRP, Joseph Ringo (katikati) 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...