Na Ashraf Said, Globu ya jamii.
Tasisi
ya Femina Hip imeanzisha kampeni yake mpya inayokwenda kwa jina la
Nguvu ya Binti ili kumsaidia msichana anapokuwa katika siku zake
.
Akizungumza
na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam leo, Lydia Charles amesema
kuwa Femina Hip imezindua kampeni ya Nguvu ya Binti ambayo itawakilishwa
na wasichana wenye historia,Tabia, na uzoefu tofauti .
“
timu mpya ya nguvu ya binti itakuwa na sauti ya wasichana wote nchini
Tanzania , wakichimbua , Kujadili na kujaribu kutatua changamoto na
vikwazo mbalimbali kwa pamoja” amesema.
Amesema kuwa wasichana hao watakuwa mawakili kwa mambo ya kijamii, Kiuchumi na kisiasa.
Ameliza
kwa kusema kuwa Femina Hip pamoja na wasichana wa kundi hilo wanamini
kwamba ni lazima kufanya kazi pamoja , kufunguka na kuzungumza kuhusiana
na hedhi ,maumivu wakati wa hedhi , Usafi wa miiko inayousishwa na
hedhi kwa kushirikisha walimu , wazazi, walezi na Wanaume pia .
Mratibu wa
programu ya Nguvu ya Binti , Lydia Charles akizungumza na Waandishi wa
Habari juu ya mpango wao wa kuwawezesha wanawake wanapokuwa katika siku
zao leo katika ofisi zao katika eneo la Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi wa Kays Hygien, Sauda Simba akizungumzia kuhusu kampuni ya Femina iliyodhamini programu hiyo
Sehemu ya Waandishi wa wakufuatilia mkutano
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...