Na Thomas William,Morogoro.
Usajili na Utambuzi wa watu katika mkoa wa Morogoro umezinduliwa rasmi Septemba 20, 2014 na Mkuu wa Mkoa wa huo, Joel Bendera katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa ya Morogoro.

Akizindua zoezi hilo aliwasisitiza wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa mamlaka za Serikali za Mitaa, makatibu tawala wilaya na viongozi wote kufikia ngazi ya kijiji na mtaa kuhakikisha kwamba wanashiriki kikamilifu katika kufanikisha usajili wa watu katika mkoa wake.

Alisema viongozi na watendaji wote katika mkoa huo wanatakiwa kuweka uzalendo mbele katika suala hilo na kuhakikisha kwamba hakuna wageni wanaopata vitambulisho vya taifa ambayo ni vya raia.

Zoezi hili ambalo linawahusu wananchi na wakazi wa wilaya zote za Morogoro ambazo ni Morogoro Mjini, Morogoro Vijijini, Mvomero, Kilosa, Kilombero, Gairo, na Ulanga wenye umri wa miaka 18 na zaidi linafanyika kwa siku saba.

Ili kusajiliwa mwombaji anatakiwa kufika katika kituo cha usajili ukiwa na nyaraka muhimu zinakazokutambulisha mathalan, cheti cha kuzaliwa, kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, Cheti cha Elimu ya Msingi, Sekondari au Chuo, Leseni ya Udereva, Kadi ya kupigia Kura, Pasipoti na Kadi ya Bima ya Afya. Wageni wanatakiwa kuwa nakala ya Pasipoti ya nchi wanazotoka na kibali cha kuishi nchini.

Aidha, mwombaji anakumbushwa kuhakikisha jina lake limesajiliwa katika rejesta ya makazi iliyopo katika Serikali ya Mtaa/Kijiji kabla ya kuanza taratibu za usajili. Vituo vitafunguliwa asubuhi saa 2:00 hadi saa 11:00 jioni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...