Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Mh. Ummy Mwalimu mwishoni mwa wiki amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Mkinga na Pangani kuhimiza wanawake kujiandikisha na kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuunga mkono juhudi za Serikali katika ujenzi wa Maabara.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu akikabidhi kadi ya (UWT) kwa Bi. Halima Kassim mmoja wa wanachama wapya katika Kata ya Maramba, Wilaya ya Mkinga.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wapya wa UWT mara baada ya kuwakabidhi kadi zao. Waliosimama kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Mkinga, Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Bi. Mboni Mgaza na Mbunge wa Viti Maalumu Al-Shymaa Kwegyir.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Mh. Ummy Mwalimu (Wa nne kutoka kulia) akipata maelezo ya ujenzi wa maabara kutoka kwa Mwalimu Cyprian Taabani kutoka Shule ya Sekondari Daluni, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Daluni Mwanakombo Gobeto.
Mh. Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga akikabidhi bati (50) kwa Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi. Hafsa Mtasiwa ikiwa ni jitihada za kuunga mkono ujenzi wa maabara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...