KANISA la Assemblies of God Tanzania (TAG) limewapatia pikipiki 400 waangalizi wa majimbo 33 nchini ya Kanisa hilo,ili kuwawezesha kufanikisha utekelezaji wa malengo makuu kumi ya dira ya maendeleo ya kanisa hilo,ili ifikapo mwaka 2018, utekelezaji wa malengo hayo yote yawe yamekamilika.

Akizungumza kwa niaba ya waangalizi waliopokea usafiri huo wa pikipiki,Mchungaji Kalebi Patrick Maumbuka wa kanisa la TAG, Ikungi Mkoani Singida alisema usafiri huo wa pikipiki utawasaidia sana kutangaza neno la Mungu kwa haraka zaidi, kwani awali walikuwa wakitegemea usafiri wa mabasi ambayo yalichangia kuwakwamisha kufikisha ujumbe wa neno la mungu kwa wakati muafaka.
Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Bwana John Mtokambali (wa kwanza kutoka kulia) akimkabidhi mmoja wa waangalizi wa kanisa wa Mkoani Singida pikipiki kwa ajili ya kuwawezesha kutangaza neon la Mungu kwenye maeneo yao.

Askofu Mkuu wa Kanisa la TAG, Bwana John Mtokambali akihubiri neno la mungu kwa waumini wa kanisa hilo waliohudhuria kwenye hafla za kuwakabidhi vyombo vya usafiri vitakavyowasaidia kuharakisha kulifikisha neno la mungu.
baadhi ya waumini wa kanisa la TAG wakiwa kwenye hafla ya makabaidhiano ya vyombo vya usafiri vya waangalizi wa makanisa nchini,sherehe hiyo ilifanyika mjini Singida.
Jengo la Kanisa la TAG lililopo katika kata ya Mandewa, wilaya ya Singida mjini kulikofanyika hafla ya kuwakabidhi waangalizi wa makanisa vyombo vya usafiri kwa ajili ya kuharakisha usambazaji wa neon la Mungu kwenye maeneo yao.Picha zote na Jumbe Ismailly

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...